• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Kamati ya Fedha Yakagua Miradi ya Maendeleo

Posted on: August 29th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango leo imekagua baadhi ya miradi ya maendeleo wilayani Mpwapwa katika kata za Berege, Mpwapwa Mjini, Chunyu, na Mazae. Miradi iliyotembelewa ni pamoja na Ujenzi wa Mkataba na Bwaro katika Shule ya Sekondari Mazae kata ya Mazae, Ukaguzi wa Magari mabovu yaliyopaki katika yadi ya Idara ya Ujenzi,  ujenzi wa madarasa mawili katika shule ya Msingi Msagali kata ya Chunyu, na ujenzi wa maktaba moja, madarasa mawili na bwalo la chakula katika shule ya sekondari Berege katika kata ya Berege.
Ukaguzi huo wa miradi umeongozwa na Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Mhe. George Fuime pamoja na wajumbe wa Kamati ya Fedha na wataalam tako Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa.

Katika Ukaguzi wa Magari sita mabovu ya Halmashauri yaliyopaki kwa muda mrefu katika yadi ya Ujenzi yamegundulika kuwa mengi ni mabovu sana, pia ni gharama kubwa kuyatengeneza na hivyo Kamati ya Fedha imependekeza kuwa ufanyika utaratibu magari haya yauzwe kwa sababu Halmashauri haina fedha ya kuweza kuyafufua. Pendekezo hilo la kuuza magari haya limejiri baada ya kukagua na kubaini ubovu wa magari hayo ambapo Halmashauri hayawezi kuyafufua kwa kuwa gharama yake ni kubwa.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wakikagua magari mabovu katika yadi ya Ujenzi

Aidha wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wamempongeza Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msagali Ndugu. Medard Mgube Tuju kwa usimamizi mzuri wa madarasa mawili yaliyojengwa kwa ufadhiri wa Mfuko wa Elimu Lipa kutookana na Matokeo (EP4R) ambapo amefanikiwa kukamilisha madarasa hayo kwa wakati na kufuata miongozo ya matumizi ya fedha zilizotolewa ambazo zilikuwa jumla ya  Tsh. 25,000,000/= Kwa sasa madarasa hayo yapo tayati kwa matumizi ana kamati ya fedha imeshauri kuwa madarasa haya kwa kuwa yanaumeme na madirisha ya vioo ni bora wakasomea wanafunzi wa madarasa ya juu kama darasa la nne, tano, sita na saba kwa kuwa wanauelewa na wanaweza kutunza miundombino ya madarasa haya.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wakisomewa taarifa ya Ujenzi wa Madarasa Mawili katika Shule ya Msingi Msagali

Ukaguzi wa Miradi umeendelea katika Shule ya Sekondari Berege ambapo  kuna ujenzi wa  Madasa mawili, maktaba moja na bwaro unaendelea. Japo katika maeneo mengi ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa majengo kama haya yameshakamilika na mengine yapo katika hatu ya umaliziaji ila hapa katika shule ya Sekondari Berege ujenzi bado unasuasua sana. Kufuatia hali hiyo Kamati ya Fedha imekufanya kikao na kamati ya ujenzi, walimu, na mafundi kujua changamoto zilizopo ambapo Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo ameeleza kuwashida kubwa ni kuwa fedha zilifungwa tangu tarehe 30/06/2018 wakati mwaka wa fedha ulipoisha.  Pia Afisa Mipango wa Wilaya ya Mpwapwa Ndugu. Nackam Nchimbi ameeleza kuwa kwa sasa jitihada za kuingiza vifungu vya bakaa katika mfumo wa FFARS ili kuweza kusaidia fedha zilizobaki zilipwe na kazi hii iendelee vizuri na iishe kwa wakati.
Kutokana na maelezo ya matumaini ya Afisa Mipango wa Wilaya, kamati ya Fedha imeagiza kuwa ifikapo tarehe 25/09/2019 majengoo yote yanayoendelea kujengwa yawe yameisha.

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wakifanya kikao na kamati ya Ujenzi katika Shule ya Sekondari Berege ndani ya Bwaro linaloendelea kujengwa.

Mwisho Kamati ya Fedha imempongeza fundi Mkuu anayejenga jengo la Bwaro kuwa ni fundi stadi na mbunifu, hivyo amejenga vizuri kwa kuzingatia ramani na kunyoosha kuta vizuri.


Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tangazo la Kuahirishwa kwa kikao cha Kamati ya Fedha uongozi na Mipango March 31, 2017
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mgao wa Pikipiki Kwa Watendaji wa Kata

    March 01, 2023
  • Mtokeo ya kidato cha nne yatangazwa

    January 29, 2023
  • Matokeo ya Mtihani Darasala nne na Kidato cha Pili 2022

    January 04, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Saba yatangazwa

    December 01, 2022
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: +255 688639341

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.