• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mkuu wa Mkoa Azuia Malipo ya Mkandarasi

Posted on: July 4th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Dkt. Binilith Mahenge amefanya ziara ya kukagua mradi wa maji katika kijiji cha Bumila kata ya Lupeta Wilayani Mpwapwa. Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa amepata fursa ya kukagua ujenzi wa tanki la maji lenye ujazo wa lita 100,000 linalotarajia kuhudumia wananchi 2204 kwa mujibu wa makadirio ya mwaka 2019. Mradi huo umejengwa na Kampuni ya Advanced Engineering Company ya Dar es salaam kwa mkataba namba LGA 023/2016-2017 ambao ulisainiwa tarehe 16/11/2017 ulitakiwa kumamilika tarehe 10/05/2018 na unafadhiliwa na Mradi wa Program ya Maji na usafi wa  Mazingira Vijijini (NRWSSP) wenye thamani ya Tsh 637,957,268.

Mpaka sasa mkandarasi amelipwa Tsh 303,879,609.99 na anadai Tsh 334,077,654 bado hajalipwa kwa sababu fedha zilichewa na hivyo kuna baadhi ya kazi hazijakamilika.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa mradi huo wa maji Bw. Ngwembele (Technician) kwa niaba ya Mhandisi Christina Msengi, kuwa ujenzi umekalika kwa kazi ya ujenzi wa jengo la COWSO, tanki, vituo 14 vya kuchota maji, nyumba ya mashine ya kusukuma maji, mlambo wa kunyeshea mifugo na mabomba yamelazwa, ila bado pampu na miundombinu ya umeme haijakamilika, hivyo mkandarasi atakamilisha.

Kazi zilizobaki ni kufunga mota, pampu na mfumo wa umeme, kazi hizo hajamalizika kwa wakati kutokana na kuchelewa kwa fedha, mara nyingi baada ya kuomba fedha huwa zinachukua muda wa miezi sita hadi kutolewa.

Baada ya kumalisha kusomewa taarifa fupi ya mradi Mkuu wa Mkoa alitoa kasoro za tanki la maji ambalo kutokana na taarifa inaonyesha kuwa limekamilika. Kasoro hiyo ni kuwa tanki hilo lina nyufa kwa chini na hivyo mkandarasi asilipwe mpaka azibe ufa huo. Dkt. Mahenge amesema "nimekagua nikiwa na Mkuu wa Wilaya, Mhandisi wa Maji wa Wilaya, mhandisi wa Tanroads na Mhandisi wa Maji mkoa tumeona tanki limepasuka chini kwa ndani na hivyo mkandarasi asilipwe fedha za tanki mpaka azibe nyufa hizo. Hii imetokana na kutomwagilia maji tu. Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa nisaidie kusimamia hili, huyu Mkandarasi asilipwe mpaka akamilishe kazi ya kuziba nyufa."

Mkuu wa Mkoa ameahidi kuwa atawasiliana na Waziri wa Maji ili fedha zikiombwa ziweze kutolewa kwa wakati ili miradi ya maji iweze kukamilika kwa wakati.

Pia Mkuu wa Mkoa amewataka wahandisi wa maji wa wilaya kusimamia miradi ya maji kwa ukamilifu ili kuweza kuwa na miradi inayodumu na endelevu. Akitolea mfano wa tanki hili la Bumila kupasuka chini ni kwa sababu ya kutosimamia vizuri kwa kuwa kosa lililofanyika hapa ni kutokumwagilia maji ya kutosha ndio maana nyufa zimetokea.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tangazo la Kuahirishwa kwa kikao cha Kamati ya Fedha uongozi na Mipango March 31, 2017
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mgao wa Pikipiki Kwa Watendaji wa Kata

    March 01, 2023
  • Mtokeo ya kidato cha nne yatangazwa

    January 29, 2023
  • Matokeo ya Mtihani Darasala nne na Kidato cha Pili 2022

    January 04, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Saba yatangazwa

    December 01, 2022
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: +255 688639341

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.