• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Mkuu wa Wilaya Ahamasisha Wananchi Kufanya Mazoezi

Posted on: January 12th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri leo amewahamasisha wananchi wa Mpwapwa kufanya mazoezi ya viungo na riadha kama ilivyokawaida  kila Jumamosi ya wiki ya pili ya kila mwezi kuwa na mazoezi ambayo yamefanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chazunga Wilayani Mpwapwa.

Aidha katika mazoezi ya leo yamehudhuriwa na Katibu Tawala wa Wilaya Ndug. Sarah Komba, Afisa Usalama wa Taifa Ndug. Said, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mpwapwa Ndug. Paul Mamba Sweya, wakuu wa idara, taasisi pamoja na wananchi kwa ujumla, wamefanya mazoezi ya ziungo kwa pamoja.

Mazoezi hayo yameongozwa na Mwalimu wa Michezo ambaye pia ni Afisa Utamaduni na Michezo Wilaya Ndug. Waziri Lwimbo kwa kutoa mazoezi mbalimbali ya viungo kwa watu wote waliohudhuria katika Viwanja vya Chazungwa.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri (wa tatu kulia), Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Sarah Komba (wa pili kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Paul Sweya (wa kwanza Kulia) wakiwa katika mazoezi ya viungo kwenye Viwanja vya Chazungwa kata ya Mpwapwa Mjini.

Baada ya kumaliza mazoezi Mkuu wa Wilaya amepata fursa ya kuzungumza na wananchi waliohudhuria katika mazoezi hayo kuwa "Kwanza nimefurahishwa sana na mwitikio mkubwa wa watu kujitokeza kwa wingi katika kuthamini mazoezi, hii inaonyesha kuwa elimu na hamasa iliyotolewa juu ya mazoezi ni tiba kiafya imeanza kueleweka vizuri. Kwa ujumla mazoezi ni tiba kiafya na mara nyingi husaidia kuondoa msongo wa mawazo, matatizo ya shinikizo la damu (blood pressure) na kuuweka mwili kuwa imara wakati wote" ameeleza Mkuu wa Wilaya Mhe. Shekimweri.

Pia ameongeza kuwa anawashukuru wakuu wa taasisi, idara, vitengo na wananchi kwa ujumla kuhudhuria katika mazoezi haya na kusema kuwa "Afya ni Mtaji wetu katika kufanyakazi kwa kuwa imara bila maradhi".

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri akizungumza na wananchi waliohudhuria katika mazoezi ya viungo kwenye Viwanja vya Chazungwa kata ya Mpwapwa Mjini.

Kwa upande mwingine Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa amezindua Klabu ya Riadha ya Kikundi cha Mtaa wa Kikombo Road katika Kata ya Mpwapwa Mjini Wilayani Mpwapwa. Uzinduzi huo umefanyika katika Viwanja vya Shule ya Msingi Chazungwa mara tu baada ya mazoezi kumalizika. Kikundi hiki kinachojulikana kwa Jina la Kikombo Road Jogging Club kimeanzaishwa na wanachama wa kikundi hicho wapatao 20 na kinafadhiriwa na Ndug. Said, Afisa Usalama wa Taifa Wilaya ya Mpwapwa pamoja na Ndug. Sarah Komba, Katibu Tawala Wilaya ya Mpwapwa. Kikundi hiki kilianzishwa tangu mwaka 2018 baada ya Serikali kutoa tamko la kuwa na Mazoezi kwa wananchi wote Nchini kwa siku ya jumamosi ya wiki ya pili ya kila mwezi ili kuunga mkono jitihada za viongozi wa Serikali za kuanzisha siku maalum kwa ajili ya mazoezi. Pia kikundi kunajihusisha na michezo ya mpira wa miguu, kikapu, riadha na mazoezi ya viungo. Kikundi hiki kina malengo ya kuanzisha michango ya ihari, kujifunza michezo mbalimbali, nje ya wilaya akaunti, kufanya mashindando na vikundi vingine vitakavyoundwa ndanina nje ya wilaya. 

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri, Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Sarah Komba na Afisa Usalama Wa Taifa Wilaya ya Mpwapwa Ndug. Said  pamoja na Wanachama wa Kikombo Roaad Jogging Club wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya uzinduzi wa club hiyo kwenye Viwanja vya Chazungwa kata ya Mpwapwa Mjini.

Mkuu wa Wilaya ametoa rai kwa wananchi wa Mpwapwa kuunda Jogging Club kila mtaa na hapa anasema "Natamani kila mtaa kuwa na Jogging Club mfano Mtaa wa Mwanakianga, Igovu, National, Majengo, Mji Mpya nk. Mimi nitakuwa bega kwa bega nanyi kwa namna yoyote ya kuunga mkono suala hili".

Mkuu wa Wilaya ametoa Wito kwa viongozi wote wa mitaa kuanzisha Jogging Club katika mitaa yao kwa kuwahusisha wananchi na watumishi wote wanawake na wanaume.

               Walimu wa michezo Ndug. Waziri Lwimbo (kusho) na Ndug. Mchasi (kulia) wakitoa mazoezi ya viungo katika Uwanja wa Chazungwa Mpwapwa Mjini

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tangazo la Kuahirishwa kwa kikao cha Kamati ya Fedha uongozi na Mipango March 31, 2017
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mgao wa Pikipiki Kwa Watendaji wa Kata

    March 01, 2023
  • Mtokeo ya kidato cha nne yatangazwa

    January 29, 2023
  • Matokeo ya Mtihani Darasala nne na Kidato cha Pili 2022

    January 04, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Saba yatangazwa

    December 01, 2022
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: +255 688639341

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.