• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Mpwapwa District Council
Mpwapwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
        • Fedha
        • Biashara
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Ufugaji na Uvuvi
      • Ardhi na Mali asili
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Usafi na Mazingira
      • Utawala na Utumishi
    • Vitengo
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Habari Mawasiliano na Tehama
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Kitengo cha Nyuki
    • Mamlaka
      • Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mpwapwa
      • Mamlaka ya Maji Mpwapwa
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uchimbaji wa Madini
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti UKIMWI
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashuri
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa mbali mbali
    • Fomu za Maombi
    • Miongozo mbali mbali
    • Simulizi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video mbali mbali
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Habari

Wananchi wa Mpwapwa Watekeleza Agizo la Makamu wa Rais

Posted on: July 13th, 2019

(Na: Shaibu J. Masasi, Afisa TEHAMA - Mpwapwa)

Wananchi wa Wilaya ya Mpwapwa wameamua kutekeleza agizo la Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hasani, Kwa wananchi wote Nchini kufanya mazoezi kila jumamosi wiki ya pili ya kila mwezi.

Wananchi hao wamejitokeza kwa wingi katika mazoezi yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Chazungwa yakiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Jabir Shekimweri ambaye amejitahidi kuwahamasisha wananchi kuwa na utamaduni wa kufanya mazoezi tangu agizo lilipotolewa. 

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Shekimweri amewasisitiza wananchi wa Mpwapwa kufanya mazoezi kila siku wanapopata muda iwe jioni au asubuhi ili kujiimarisha kiafya. Pia aliwahamasisha wananchi kwa kila mtaa na kata kuunda Klabu ya Riadha (Jogging Clubs). 

Aidha, baada ya Mkuu wa Wilaya kuhamasisha uundwaji wa klabu za riadha, mwitikio umukuwa mkubwa na mpaka sasa kuna klabu 12 hai, klabu hizo ni National jogging Club, Kikombo, Mwanakianga, Hazina, TTC, Mpwapwa Sec, Ilolo, Igovu, Mjini kati, Mji mpya, Majengo na Ng'ambo.

Katika mazoezi yanayofanyika kila mwezi katika Jumamosi ya wiki ya pili ya Mwezi kama agizo linavyosema, kumekuwa na walimu wa michezo na madaktari wakielimisha wananchi umuhimu wa kifanya mazoezi kiafya na namna ya kufanya mazoezi bila kuleta madhara kwa mtu.

Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe. Shekimweri ametumia fursa hii ya mkusanyiko wa wananchi kuwaomba kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kuleta maendeleo. Pia amewataka kufanya mazoezi ili kuwa na afya ili waweze kufanya shughuli za maendeleo ikiwemo kilimo, biashara na kujitolea katika kuchangia nguvukazi katika miradi ya serikali katika maeneo yao. 

Vilevile ameipongeza Shule ya Sekondari Mpwapwa kwa kuwa ya kwanza kimkoa kwa kufaulisha vizuri matokeo ya kidato cha sita kwa mitihani ya mwaka 2019. Hivyo amewataka walimu na wanafunzi kuendelea kuweka jitihada ili kuishikilia nafasi hii kwa miaka ijayo na hata kuwa wa kwanza kitaifa.

Matangazo

  • Tangazo la kuitwa kwenye usahili MpwapwaDC June 27, 2022
  • Tangazo la Nafasi za Kazi Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa May 2022 May 31, 2022
  • Tangazo la kuahirishwa kwa Usahili Halmashauri ya Mpwapwa June 22, 2022
  • Tangazo la Kuahirishwa kwa kikao cha Kamati ya Fedha uongozi na Mipango March 31, 2017
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mgao wa Pikipiki Kwa Watendaji wa Kata

    March 01, 2023
  • Mtokeo ya kidato cha nne yatangazwa

    January 29, 2023
  • Matokeo ya Mtihani Darasala nne na Kidato cha Pili 2022

    January 04, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Saba yatangazwa

    December 01, 2022
  • Tazama zote

Video

Video ya Mpango wa Uuzaji wa Viwanja Eneo la Mazae Block "E" katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa -2020
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Ramani ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa
  • Muundo wa Baraza la Waheshimiwa Madiwani
  • Ratiba ya Vikao vya Madiwani

Viunganishi Linganishi

  • Baraza la Mitihani Tanzania
  • Wizara ya Fedha na Mipango
  • Utumishi portal
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu Teknolojia na Sayansi
  • Sekretarieti ya Ajira

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mpwapwa - Dodoma, Tanzania

    Anwani: S.L.P 12

    Simu: 255 26 2320122/2320

    Simu ya Kiganjani: +255 688639341

    Barua pepe: info@mpwapwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovutii

Copyright © 2021 Mpwapwa District Council . All rights reserved.